Waziri Mkuu wa Lebanon atoa wito kwa nchi kuchukua msimamo wa wazi juu ya 'mauaji ya kutisha'
Waziri Mkuu wa Lebanon atoa wito kwa nchi kuchukua msimamo wa wazi juu ya 'mauaji ya kutisha'

Chanzo cha picha, EPA-EFE/REX/Shutterstock
Waziri Mkuu wa Lebanon ametoa wito kwa jumuiya ya kimataifa "kuchukua msimamo wa wazi" juu ya kile anachoita "mauaji haya ya kutisha" katika taarifa iliyochapishwa leo .
Waziri Mkuu Najib Mikati anasema alikuwa na nia ya kusafiri kwenda New York kushiriki katika Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, lakini aliamua kutosafiri baada ya matukio ya wiki hii.
"Ninasisitiza kwamba hakuna kipaumbele kwa sasa ambacho ni cha juu zaidi kuliko kukomesha mauaji yanayofanywa na adui - Israel na aina mbalimbali za vita wanavyoendesha," ilisema taarifa hiyo.
"Pia natoa wito kwa jumuiya ya kimataifa na ulimwengu kuchukua msimamowa wazi kuhusu mauaji haya ya kutisha."
Mikati pia anatoa wito wa "kupitishwa kwa sheria za kimataifa ili kupunguza njia za kiteknolojia za kiraia kutoka kwa malengo ya kijeshi na vita" kutokana na mashambulizi ya vifaa vya mawasiliano nchini mwake.
Mashariki ya Kati ipo 'kwenye ukingo wa janga linalokaribia'
Jeanine Hennis, mratibu maalum wa Umoja wa Mataifa kwa ajili ya Lebanon, ametoa onyo kwa Israel na Hezbollah baada ya mapigano ya jana usiku.
Alisema: "Kwa kuwa eneo liko ukingoni mwa janga linalokaribia, haliwezi kuelezewa vya kutosha: HAKUNA suluhu la kijeshi ambalo litafanya kila upande kuwa salama."
Comments
Post a Comment