Takriban watu 51 wamefariki katika mlipuko wa mgodi wa makaa ya mawe nchini Iran
Takriban watu 51 wamefariki katika mlipuko wa mgodi wa makaa ya mawe nchini Iran

Chanzo cha picha, APTN
Mlipuko uliosababishwa na uvujaji wa gesi kwenye mgodi wa makaa ya mawe mashariki mwa Iran umeua takriban watu 51, vyombo vya habari vya serikali vilisema Jumapili.
Zaidi ya wengine 20 walijeruhiwa baada ya mlipuko huo katika jimbo la Khorasan Kusini.
Inaripotiwa kusababishwa na mlipuko wa gesi ya methane katika vitalu viwili vya mgodi huko Tabas, kilomita 540 (maili 335) kusini mashariki mwa mji mkuu Tehran.
Mlipuko huo ulitokea saa 21:00 kwa saa za ndani (17:30 GMT) siku ya Jumamosi, vyombo vya habari vya serikali vilisema.
Gavana wa Khorasan Kusini Javad Ghenaatzadeh alisema kulikuwa na wafanyikazi 69 kwenye vitalu wakati wa mlipuko huo.
Kwa mujibu wa shirika la habari la AP, alisema: "Kulikuwa na mlipuko na kwa bahati mbaya watu 69 walikuwa wakifanya kazi katika vitalu vya B na C vya mgodi wa Madanjoo.
"Katika kitalu C kulikuwa na watu 22 na katika kitalu B kulikuwa na watu 47."
Bado haijafahamika ni watu wangapi ambao bado wako hai na wamenaswa ndani ya mgodi.
Vyombo vya habari vya serikali sasa vimerekebisha idadi yake ya awali ya vifo 30.
"Idadi ya wafanyikazi waliokufa iliongezeka hadi 51 na idadi ya waliojeruhiwa iliongezeka hadi 20," shirika rasmi la habari la IRNA liliripoti.
Kwa mujibu wa shirika la habari la Reuters, Rais wa Iran Masoud Pezeshkian alitoa rambirambi kwa familia za wawlioathiriwa.
"Nilizungumza na mawaziri na tutafanya kila tuwezalo kufuatilia," Pezeshkian alisema katika ujumbe wa televisheni.
Comments
Post a Comment