Israel yaamuru kufungwa kwa siku 45 kwa ofisi ya Al Jazeera Ukingo wa Magharibi

 

Israel yaamuru kufungwa kwa siku 45 kwa ofisi ya Al Jazeera Ukingo wa Magharibi

th

Chanzo cha picha, AlJAZEERA

Vikosi vya Israel vimevamia ofisi za shirika la utangazaji la Al Jazeera huko Ramallah, katika Ukingo wa Magharibi unaokaliwa kwa mabavu na kuamuru kufungwa kwa muda wa siku 45.

Wanajeshi wa Israel wenye silaha na waliojifunika nyuso zao waliingia ndani ya jengo hilo mapema Jumapili wakati wa matangazo ya moja kwa moja.

Watazamaji walitazama wanajeshi wakitoa agizo la kufungwa kwa mkuu wa ofisi hiyo katika Ukingo wa Magharibi Walid al-Omari ambaye aliisoma moja kwa moja ujumbe huo hewani.

Israel ilivamia ofisi za Al Jazeera huko Nazareth na Jerusalem Mashariki inayokaliwa kwa mabavu mwezi Mei baada ya kulielezea shirika hilo la utangazaji lenye makao yake Qatar kuwa tishio kwa usalama wa taifa.

"Kulenga waandishi wa habari kwa njia hii kila mara kunalenga kufuta ukweli na kuzuia watu kusikia ukweli," Omari alisema katika maoni yaliyoripotiwa na mwajiri wake.

Wanajeshi hao walichukua maikrofoni na kamera ya mwisho nje ya barabara ya ofisi hizo na kumlazimisha Omari kutoka nje ya ofisi, mwandishi wa habari wa Al Jazeera Mohammad Alsaafin alisema.

Akichapisha kuhusu uvamizi huo kwenye mitandao ya kijamii, Alsaafin alisema wanajeshi hao pia waling'oa bango la Shireen Abu Aqla - ripota wa Al Jazeera ambaye aliuawa wakati akiripoti uvamizi wa vikosi vya Israel katika Ukingo wa Magharibi.

Aljazeera na mashuhuda wa wakati huo walisema mwandishi huyo wa habari Mpalestina mwenye uraia wa Marekani alipigwa risasi na wanajeshi wa Israel. Hapo awali Israel ilidai kuwa alipigwa risasi na Mpalestina, hata hivyo miezi kadhaa baadaye ilihitimisha kuwa kulikuwa na "uwezekano mkubwa" kwamba mmoja wa askari wake alimuua.

Comments

Popular posts from this blog

Israel yazuia mikusanyiko kaskazini mwa nchi huku ikiendelea kushambulia Hezbollah

Mashambulizi ya Israel huko Lebanon yana athari gani?

Korea Kaskazini kupanua silaha za nyuklia